Bwana Yesu Kristo asifiwe sana. mimi na familia yangu tunamshukuru sana Mungu. Siku zinakimbia huu ni mwezi wa tatu. Naamini umeanza kuuzoea na kuona ni nini cha kufanya kwa mwaka huu.
Mwezi uliopita tumekua na semina nzuri sana hapo Iyunga kwenye kanisa la Moravian tulikua na semina nzuri sana. Mwezi huu wa tatu tutaanza kupokea salamu mpya.
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4,"writingDirection":1}}">Tutakua na salamu ambazo ndani yake kutakua na mambo ya kiutu uzima, yaani ni masomo ya watu wazima. Naamini tutakapoanza kuzipokea utagundua ni masomo ambayo hatujazoea kuyasikia. </span>
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4,"writingDirection":1}}">Sasa nataka nikupe kazi ya kufanya. Niombee kwa Mungu ili anipatie neno ambalo utaelewa na utakua kiroho na kiuchumi. Mwombe Roho Mtakatifu ili atufundishe na kutupa kuelewa.</span>
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4,"writingDirection":1}}">Hebu tuanze kupokea salamu za mwezi wa tatu </span>
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4}}">JIFUNZE KUTAKA KARAMA AU KUOMBA MUNGU AKUPE KARAMA YA UNABII ILI UPATE KUFANIKIWA KIROHO WEWE NA WATU WENGINE (SEHEMU YA KWANZA) </span>
UTANGULIZI:
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4}}">Karibu sana ndugu yangu ili tupate kujifunza somo hili..Somo hili ni miongoni mwa masomo ambayo ni adimu sana kuyakuta yakifundishwa. Somo hili ni somo ambalo ndani yake limebeba malengo haya yafuatayo. </span>
<span data-tt="{"paragraphStyle":{"alignment":4}}">MALENGO YA SOMO HILI </span>
- Kukutengenezea vema ushirika kati yako na Mungu Ushirika wetu na Mungu umefungwa kwenye neno …Mungu anapotupa somo hili amekusudia kuona unakua na ushirika mzuri na Mungu
- Kukusaidia kupewa vema maelekezo au maagizo kutoka kwa Mungu Mungu anatabia ya kutupa maelekezo, ndani ya somo hili tutajua njia ambazo Mungu anazitumia ili kutupa maelekezo. Ili wewe na mimi tufanikiwe ni lazima tujifunze kumsikiliza Mungu anasema nini ili tupate miongozo kutoka kwake katika kila tunachokifanya
- Kukuwezesha kusikia sauti na neno la Mungu Unaposoma Biblia unajifunza kuwa. Unaweza kusikiliza neno la Mungu ambalo halijabebwa na sauti ya Mungu.
- Kukupatia maarifa,hekima,na ufahamu kutoka kwa Mungu Ili tufanikiwe katika mambo yoote tunatakiwa tujifunze kusikiliza neno la Mungu. Ndani ya somo hili tutajifunza namna ya kulipokea neno la Mungu ambalo ndani yake kuna maarifa na ufahamu yatokayo kutoka kwa Mungu.
- App yetu ya huduma yenye jina “MWAKATWILA (HUSONEMU)” utaipata Play Store ambapo kuna masomo mengi sana hapo.
- Tovuti yetu ya www. mwakatwila. org
- YouTube – Mwakatwila au HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU (HUSONEMU).
- Facebook ingia katika hiyo tovuti (website) yetu utaona alama ya Facebook (f) “like” na utapata maelezo ya kujiunga au ingia Facebook halafu andika “SOMA NENO LA MUNGU”
- Instagram ingia Instagram app halafu andika “Steven Mwakatwila”
- DVDs au CDs
- VITABU. Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733, ili kupata VITABU, DVD & CD.
- Kwa njia ya REDIO: – Utapata mafundisho yetu kwa redio zifuatazo:-
- Rungwe FM 102. 5 Kila siku ya Jumapili saa tatu mpaka saa nne usiku.
- Baraka FM 107. 7 Kila siku ya Jumanne saa kumi na mbili jioni mpaka saa moja usiku.
- Bomba FM 104. 1 Kila siku ya Ijumaa saa tatu usiku mpaka saa nne usiku.