Bwana Yesu Kristo asifiwe.. Tunamshukuru Mungu atupendaye na ni mwema kila saa…
Tumepewa mwezi huu wa sita kwa neema yake. .
Katika mwezi uliopita tulikua na semina Jijini Mbeya kwenye viwanja vya Otu. Tulikua na semina nzuri sana. Mwezi huu tunararajia kuwa na semina huko Dodoma mvumi,tutaenda Manyoni,na tutaenda Itigi..
Tuombeeni sana.
Hebu tuanze kuzipokea salamu za mwezi huu wa sita.. Kumbuka tuna salamu zenye kichwa
JIFUNZE KUTAKA KARAMA AU KUOMBA MUNGU AKUPE KARAMA YA MIUJIZA NA UPONYAJI ( SEHEMU YA PILI)
4: MUNGU ANAUTUMIA MUUJIZA ILI WATU WASHANGAE
Neno mshangao maana yake ni hisia au ni jambo lisilotarajiwa au lisilo la kawaida.. Watu wanapokutana na jambo lisilo la kawaida hujikuta wakishangaa na hata kuogopa au hata kumuona Mungu ni mkuu mnoooo…
Mungu hutumia miujiza ili kuwashangaza wanadamu au watu, wawe wanaomwamini na wasio mwamini.
Mwanadamu anatafuta kuyaona ma,bo yasiyo ya kawaida katika maisha yake. Sasa sikia unapoitwa umtumikie Mungu lazima ujifunze umruhusu Mungu afanye mambo ya kushangaza ili wanadamu au wamuone Mungu ni wa kushangaza.
Ngoja nijaribu, ukimtazama mwanadamu kila siku anaongezewa maarifa na akili, kuna mambo wanadamu kwa kutumia akili waliyopewa na Mungu wanavumbua mambo mengi ya kushangaza.
Sasa unapowaambia watu kuwa Mungu ni Mungu wa kushangaza unatakiwa ujue kuwa kwasababu kuna mambo mengi ya kushangaza wanayoifanya wanadamu wewe mwenyewe lazima umruhusu Mungu afanye mambo ambayo mwanadamu hawezi kuyafanya na ashangae.
Ukikutana wanasansi wengi ni ngumu kuwaona wakiamini kuwa Mungu yupo, wao wanafanya mambo ya kushangaza sana kwa kutumia sayansi.
Sasa sikia ili watu au wanadamu waanze kumuona Mungu ni wa kushangaza ni pale Mungu atende muujiza ili hata hao wanasayansi nk washangae na kumuona Mungu kuwa ni mkuu.
Ngoja nijaribu, unajua leo hii wanadamu wengi hawaoni Mungu kuwa ni mkuu na wakushangaza ni pale wanapoiangalia mambo ya kushangaza ya wachawi na waganga na miungu mingine.
Umewahi jiuliza swali kwanini kanisa haliongezeki nk? Sikia ni kwasababu kanisani leo hii hawamuoni Mungu kuwa yupo. Hawaoni mambo ya kushangaza, wengi wanaenda kuitafuta hiyo miujiza na kushangaa kwa miungu na wachawi.
Ngoja nijaribu. Sikia wanadamu wanatafuta kushangaa au kukutana na vitu vipya visivyo vya kawaida. Kama kanisa hatita tafuta au kutaka miujiza ndani ya kanisa fahamu kanisa hilo halitaongezeka na litakufa.
Kama unafikiri nakutania wewe lianglie kanisa la huko ulaya utagundua moja ya sababu ya kufa ni hili ninalokuambia. Kanisa likosa miujiza linakuwa ni kanisa lisilo na uhai…
Ngoja nijaribu,yaangalie yale madhehebu ambayo yanamaneno mengi lakini hawamuoni Mungu akitenda kazi yaani miujiza fuatilia baada ya miaka ijayo yana kufa au kuzimia kisa ni hiki ninachokuambia.
Miujizani ni karama ya nguvu za Mungu zinazotoa ishara yakuwa Mungu yupo hai anaishi na anafanya kazi na watumishi wake.
Kanisa likipoteza karama ya uponyaji nk fahamu watu wataenda kutafuta uponyaji kwa miungu ili huko wakapone na kushangaa.
Sauli alipopteza muujiza wa kuwasiliana na Mungu alienda kutafuta muujiza huo wa kuongozwa kwa wenye mapepo.
Hata leo ndiyo hivyo hivyo.. ukimuona mtumishi anayetumika na miujiza fahamu watu watamtafuta ili tu wakashangae shangae..
Miujiza inaleta watu washangae … Angalie mistari hii “39 Alipokwisha kuingia, akawaambia, Mbona mnafanya ghasia na kulia? Kijana hakufa, bali amelala tu.40 Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana.41 Akamshika mkono kijana, akamwambia, Talitha, kumi; tafsiri yake, Msichana, nakuambia, Inuka.42 Mara akasimama yule kijana, akaenda; maana alikuwa amepata umri wa miaka kumi na miwili. Mara wakashangaa mshangao mkuu.”(Marko 5:39-42)
Muujiza aliofanya Bwana Yesu Kristo wa kumfufua binti huyo kila mtu alipata kushangaa..tena ushangao huo ulikuwa mkuu mnoo. Maana yake kila mtu alimuona Mungu kuwa ndiye mkuu kuliko kitu chochote
Unaposoma Biblia unaona muujiza huleta mshangao na kulifanya neno la Mungu lienee sana .
Angalia mistari hii uone. “35 Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, mtoke. Ndipo yule pepo akamwangusha katikati, akamtoka asimdhuru neno.36 Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.37 Habari zake zikaenea kila mahali katika nchi ile.”( Luka 4:35-37)
Ili neno au kazi ya Mungu ienee kila mahali atatumia mbinu hii ya muujiza. Mungu hafanyi miujiza ili kuwafurahisha watu, Mungu hufanya miujiza ili kuitangaza kazi za Mungu au mpango wa Mungu au mpango wake nk.
Sikia mpendwa ebu tubadilike tusiridhike na huduma zetu zilivyo..
Naamini umepokea kitu katika salamu hizi za mwezi huu wa sita.
Ukihitaji masomo yetu, unaweza kuyapata kwa njia zifuatazo:
1. App yetu ya huduma yenye jina “HUSONEMU (MWAKATWILA)” — inapatikana Play Store, ambapo kuna masomo mengi sana.
2. Tovuti yetu: www.mwakatwila.org
3. YouTube: HUDUMA YA SOMA NENO LA MUNGU
4. Facebook: ingia kwenye tovuti yetu uone alama ya Facebook (f), kisha “like” ili upate maelezo ya kujiunga, au tafuta “SOMA NENO LA MUNGU”
5. Instagram: tafuta “Huduma ya Soma Neno la Mungu”
6. DVDs 📀 au CDs 💿
7. Vitabu
NB: Wasiliana na mhudumu ofisini kwa namba +255 763 109 733 ili kupata vitabu, DVD na CD.
8. Kwa njia ya redio:
- Rungwe FM 102.5 MHz — Jumapili saa 3:00 hadi 4:00 usiku
- Baraka FM 107.7 MHz — Jumanne saa 12:00 jioni hadi 1:00 usiku
- Bomba FM 104.1 MHz — Ijumaa saa 3:00 hadi 4:00 usiku
9. Online Radio: radio.mwakatwila.org
Ratiba ya vipindi:
- Saa 12:00 asubuhi
- Saa 07:00 mchana
- Saa 12:00 jioni
- Saa 03:00 usiku
10. Ingia MWAKATWILA YouTube Online
Kwa mawasiliano zaidi:
+255 754 849 924
+255 756 715 222
Wako,
Mwl. Steven Mwakatwila & Beth Mwakatwila